Popular Posts

Sunday, February 28, 2016

UNAMJUA MTU MREFU KULIKO WOTE TANZANIA?

Inasemekana ni kijana mrefu kuliko wote Tanzania. Kijana huyu
 (katikati pichani) ambaye anadhaniwa ni mrefu kuliko vijana wote
 Tanzania anaishi maeneo ya Gongolamboto, Banana jijini Dar es salaam.
Kijana huyu huwa haonekani sana mitaani, lakini aliingia mjini siku hiyo 
 na kuleta kizaa zaa kikubwa pale alipoibuka mitaa ya Aggrey, Kariakoo. 
Alikuwa kivutio kwa kila aliyemuona, alifunga mtaa watu wakimshangaa 
na kumgombania kupiga nae picha. Kila aliyetaka kupiga nae picha alitoa
 Shilingi elfu moja Tsh. 1000. 

Picha hiyo amepigwa ndani ya Kinyozi (Salon) aliyoingia kupunguza nywele
 zake na umati wa watu walikuwa nje ya kinyozi huyo kumsubiri atoke. 
Mpaka sasa hajajulikana jina lake kamili na anafanya nini. Inasemekana 
kuna watu wanamfuatilia kumsaidia umaarufu.
 
 
Ukimuangalia kwa mara ya kwanza mchezaji wa Tanzania anayecheza
 timu ya kikapu ya Oklahoma City Sounders inayoshiriki Ligi ya Kikapu
 Marekani (NBA), Hasheem Thabit unaweza kujiridhisha kwamba ni mrefu
 kuliko Watanzania wote uliowahi kuwaona. Ana futi 7.3.
Lakini mjini Bagamoyo katika Mkoa wa Pwani kwenye shule ya Lord Barden
 yupo mchezaji anayemzidi Hasheem kwa urefu akiwa na futi 7.5.
 

No comments:

Post a Comment