Popular Posts

Thursday, March 3, 2016

Bei mpya za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa imetangazwa


March 1 2016 Mamlaka ya udhibiti wa huduma za
 nishati na maji nchini (EWURA) ilitangaza bei
 mpya ya bidhaa za mafuta ya Petrol, Diesel na
 ya mafuta ya taa katika masoko yote ya jumla na
 rejareja ambapo bei hizo zitaanza kutumika kuanzia
 tarehe 2 march 2016.
Akiongea na waandishi wa habari Dar es salaam,
 Mkurugenzi wa huduma za nishati na maji (EWURA),
 Felix Ngamlagosi amesema kuanzia tarehe 2 March 
bei za mafuta zimebadilika ikilinganishwa na toleo 
lililopita la February 2016, kwa March 2016 bei ya
 rejareja za petroli imepungua Tsh 31 kwa lita sawa
 na 1.70%, Diesel imepungua Tsh 114 kwa lita sawa na
 7.10% na mafuta ya taa yamepungua kwa Tsh 234 kwa
 lita sawa na 13.75%
kwa kiasi kikubwa , kupungua huku kwa bei za mafuta
 kwenye soko la ndani kumetokana na kuendelea kushuka
 kwa bei za mafuta katika soko la dunia

No comments:

Post a Comment